Ingia / Jisajili

Waufumbua Mkono Wako

Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Zaburi

Umepakiwa na: Richard Samson

Umepakuliwa mara 1 | Umetazamwa mara 0

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 17 Mwaka B
- Katikati Dominika ya 18 Mwaka A

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Zab.145:8-9,15-18,(K)16

Waufumbua mkono wako mkono wako; wakishibisha kila kilicho hai, kilicho hai matakwa yake x2.

1. Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema.
Bwana ni mwema kwa watu wote, na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.

2. Macho ya watu wote yakuelekea wewe; nawe huwapa chakula chao wakati wake.
Waufumbua mkono mkono wako, wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.

3. Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote; na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote,
Bwana yu karibu na wote wamwitao, wote wamwitao kwa uaminifu.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa