Ingia / Jisajili

Utanijulisha Njia Ya Uzima

Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Zaburi

Umepakiwa na: Richard Samson

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 3 ya Pasaka Mwaka A

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Zab.16:1-2,5,7-11(K)11

1. Mungu, unihifadhi mimi, Kwa maana nakukimbilia Wewe. Nimemwambia Bwana, ndiwe Bwana wangu; Bwana ndiye fungu la posho langu, Na la kikombe changu; Wewe unaishika kura yangu.

2. Nitamhimidi Bwana aliyenipa shauri, Naam, mtima wangu umenifundisha usiku. Nimemweka Bwana mbele yangu daima, Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu, sitaondoshwa.

3. Kwa hiyo moyo wangu unafurahi, Nao utukufu wangu unashangilia, Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini. Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu, Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.

4. Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume, Mna mema ya milele.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa