Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson
Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Miito | Zaburi
Umepakiwa na: Richard Samson
Umepakuliwa mara 2 | Umetazamwa mara 0
Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 2 Mwaka A
- Katikati Dominika ya 2 Mwaka B
Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, tazama nimekuja kuyafanya mapenzi yako x2.
1. Nalimngoja Bwana kwa saburi,
Akaniinamia akakisikia kilio changu.
Akatia wimbo mpya kinywani mwangu
Ndio sifa zake Mungu wetu.
2. Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,
Masikio yangu umeyazibua,
Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Ndipo niliposema, Tazama nimekuja.
3. Katika gombo la chuo nimeandikiwa,
Kuyafanya mapenzi yako,
Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;
Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.
4. Nimehubiri habari za haki
Katika kusanyiko kubwa,
Sikuizuia midomo yangu;
Ee Bwana, unajua.