Ingia / Jisajili

Uhimidiwe Mungu

Mtunzi: Sebastian Don Ndibalema
> Mfahamu Zaidi Sebastian Don Ndibalema
> Tazama Nyimbo nyingine za Sebastian Don Ndibalema

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Shukrani

Umepakiwa na: Sebastian Ndibalema

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 1

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

UHIMIDIWE MUNGU

Uhimidiwe Mwenyezi Mungu uliyeumba umzi yangu,

Uhimidiwe Bwana Mungu muweza wa vyote

Uhimidiwe Mwenyezi Mungu asili ya uhai wangu, milele hata na milele uhimidiwe Mungu

Wewe unayejua kuketi kwangu, unayejua kuondoka kwangu

Unayejua kulala kwangu na kuamka kwangu

 

1.      Umeniumba mwanadamu tena na jinsi ya ajabu

Ukanileta duniani nitawale vyote

Umeniumba mimi Bwana tena kwa jinsi ya ajabu kwa sura na mfano wako ukanifinyanga

Ukanitofautisha na wanyama wa porini (hao)

Ni hayawani hawana akili wala dhamiri (Bwana) uhimidiwe Mungu

 

2.      Wako wengi walitamani kuiona siku hii, lakini wewe  Bwana uliwaita mapema

Tazama mimi sio mwema sana zaidi ya waliotangulia

Bali ni kwa neema yako Mungu wangu

 

3.      Ujaposema rudi ee mwanadamu nafsi yangu itakurudia wewe (kwani)

Hatima ya maisha yangu unaijua wewe

Na utakaposema vijito vya baraka vibubujike kuelekea kwangu

Ni nani Bwana huyo ni nani atakayepinga

 


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa