Mtunzi: Sebastian Don Ndibalema
> Mfahamu Zaidi Sebastian Don Ndibalema
> Tazama Nyimbo nyingine za Sebastian Don Ndibalema
Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Shukrani
Umepakiwa na: Sebastian Ndibalema
Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 1
Download Nota Download MidiUHIMIDIWE
MUNGU
Uhimidiwe Mwenyezi
Mungu uliyeumba umzi yangu,
Uhimidiwe Bwana Mungu
muweza wa vyote
Uhimidiwe Mwenyezi
Mungu asili ya uhai wangu, milele hata na milele uhimidiwe Mungu
Wewe unayejua kuketi
kwangu, unayejua kuondoka kwangu
Unayejua kulala kwangu
na kuamka kwangu
1. Umeniumba
mwanadamu tena na jinsi ya ajabu
Ukanileta duniani nitawale vyote
Umeniumba mimi Bwana tena kwa jinsi
ya ajabu kwa sura na mfano wako ukanifinyanga
Ukanitofautisha na wanyama wa
porini (hao)
Ni hayawani hawana akili wala
dhamiri (Bwana) uhimidiwe Mungu
2. Wako
wengi walitamani kuiona siku hii, lakini wewe
Bwana uliwaita mapema
Tazama mimi sio mwema sana zaidi ya
waliotangulia
Bali ni kwa neema yako Mungu wangu
3. Ujaposema
rudi ee mwanadamu nafsi yangu itakurudia wewe (kwani)
Hatima ya maisha yangu unaijua wewe
Na utakaposema vijito vya baraka
vibubujike kuelekea kwangu
Ni nani Bwana huyo ni nani
atakayepinga