Ingia / Jisajili

Nitakushukuru Bwana

Mtunzi: Alex Rwelamira
> Mfahamu Zaidi Alex Rwelamira
> Tazama Nyimbo nyingine za Alex Rwelamira

Makundi Nyimbo: Shukrani | Zaburi

Umepakiwa na: Alex Rwelamira

Umepakuliwa mara 57 | Umetazamwa mara 126

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
Nitakushukuru Bwana kwa moyo wangu wote nitayasimulia matendo yako matendo yote ya ajabu X2

Nitafurahi na kukushangilia (wewe) nitafurahi na kukushangilia wewe nitaliimbia jina lako wewe uliye juu wewe uliye juu X2

1. Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma hujikwaa na kuangamia mbele zako na kuangamia mbele zako

2. Kwa maana umenifanyia hukumu na haki umeketi umeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki

3. Umewakemea hao mataifa na kumwangamiza kumwangamiza mdhalimu umelifuta jina lao milele

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa