Ingia / Jisajili

Ni Neno Jema Kumshukuru Bwana

Mtunzi: Br. Stan Mkombo, Ofmcap
> Tazama Nyimbo nyingine za Br. Stan Mkombo, Ofmcap

Makundi Nyimbo: Shukrani | Zaburi

Umepakiwa na: Stanslaus Mkombo

Umepakuliwa mara 1,688 | Umetazamwa mara 6,086

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

NI NENO JEMA KUMSHUKURU BWANA (Zab 92)

[Nd. Stanslaus L. Mkombo, OFMCap]

// Ni neno je---ma kumshukuru Bwana, (Mungu wetu) na kuliimbia Jina lako ee Uliye Juu, kuzitangaza rehema zako asubuhi, na uaminifu wako wakati wa usiku.//x2

1.     I: Kwa chombo chenye nyuzi kumi, kwa kinanda na kwa mlio wa sauti tamu ya kinu-bi; (I-IV) Umenifurahisha Bwana, kwa kazi ya mikono yako; na kwa matendo yako nitashangilia.

2.     II: Wasio haki wataangamizwa milele, maana hao adui zako Bwana watapotea;

(I-IV) Watendao maovu watatawanyika wote pia.

3.     III: Lakini mwenye haki atasitawi kama mtende, atakuwa kama mwerezi wa Lebanoni; (I-IV) Waliopandwa nyumbani mwa Bwana watasitawi katika nyua zake.

4.     IV: Watazaa matunda hata wakati wa uzee, watajaa utomvu watakuwa nao ubichi; watangaze ya kuwa Bwana ni mwenye adili, (I-IV) Ndani yake Mwamba wangu hamna udhalimu.


Maoni - Toa Maoni

prosper Jul 29, 2016
prosperdoto@gmail.com

Toa Maoni yako hapa