Ingia / Jisajili

Inukeni Enyi Malango

Mtunzi: Br. Stan Mkombo, Ofmcap
> Tazama Nyimbo nyingine za Br. Stan Mkombo, Ofmcap

Makundi Nyimbo: Majilio | Matawi | Zaburi

Umepakiwa na: Stanslaus Mkombo

Umepakuliwa mara 542 | Umetazamwa mara 2,568

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

  INUKENI ENYI MALANGO                                                        [Br. Stanslaus Mkombo, OFMCap.]

//(III: Inukeni enyi malango), (wote) Inukeni enyi enyi malango ya milele, Mfalme Mtukufu apate kuingia, Yeye Bwana ni Mfalme wa Utukufu.//X2

//(I&II: Inukeni ee malango) (wote) Ya milele, (I&II Bwana Mfale Mtukufu) (wote) Apate kuingia.//x2

Mashairi

1.  Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana,/  dunia na wote wakaao ndani yake; /Maana kaiweka misingi yake juu ya bahari,/ na juu ya mito ya maji /aliithibitisha

2.  Ni nani atakayepanda mlima wa Bwana/ na kusimama patakatifu pake Bwana?/ Ni mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe;/ asiye iinua nafsi/ yake kwaubatili.

3. Atapokea atapokea baraka kwa Bwana/ na haki kwa Mungu, Mungu wa wokovu wake./ Hiki ndicho kizazi cha wakutafutao e-e Mungu;/ watafutao uso wako/ ee Mungu wa Yakobo.

4. Inukeni inukeni ee malango ya milele, Mfalme Mtukufu apate kuingia. Ni nani Mfalme Mtukufu, Ni Bwana wa Majeshi; Bwana mwenye nguvu hodari, hodari wa vita.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa