Ingia / Jisajili

Nafsi Yangu Inakuonea Kiu

Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Zaburi

Umepakiwa na: Richard Samson

Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 22 Mwaka A
- Katikati Dominika ya 32 Mwaka A

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Zab.63:1-5,7-8,(K)1a

Ee Bwana (Bwana), Mungu wangu Mungu wangu (nafsi), nafsi yangu inakuonea kiu x2.

1. Ee Mungu, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, Nafsi yangu inakuonea kiu.

Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na chovu, isiyo na maji.

2. Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, Nizione nguvu zako na utukufu wako.

Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai, Midomo yangu itakusifu.

3. Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai, Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.

Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono, Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.

4. Maana Wewe umekuwa msaada wangu, Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.

Nafsi yangu imekuandama sana, Mkono wako wa kuume unanitegemeza.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa