Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson
Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Zaburi
Umepakiwa na: Richard Samson
Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 0
Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 12 Mwaka A
Zab.69:7-9,13,16,32-34,(K)13
Kwa wingi wa fadhili zako unijibu x2
1. Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, Fedheha imenifunika uso wangu.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu.
Maana wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu yao wanaokulaumu zimenipata.
2. Nami maombi yangu nakuomba Wewe Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu,
Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.
Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa kadiri ya rehema zako unielekee.
3. Walioonewa watakapoona watafurahi; Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe.
Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji, Wala hawadharau wafunga wake.
Mbingu na nchi zimsifu; Bahari na vyote viendavyo ndani yake.