Ingia / Jisajili

Utanijulisha Njia

Mtunzi: Adolf A. Katambi
> Mfahamu Zaidi Adolf A. Katambi
> Tazama Nyimbo nyingine za Adolf A. Katambi

Makundi Nyimbo: Pasaka

Umepakiwa na: Adolf A. Katambi

Umepakuliwa mara 3 | Umetazamwa mara 8

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 3 ya Pasaka Mwaka A

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
KIITIKIO Utanijulisha njia utanijulisha njia ya uzima njia njia ya uzima. X2 MASHAIRI 1. Mungu unihifadhi mimi kwa maana nakukimbilia wewe nimemwambia Bwana ndiwe Bwana wangu Bwana ndiye fungu la posho langu na lakikombe changu wewe unaishika unaishika kura yangu. 2. Nitamhimidi Bwana aliyenipa shauri Naam mtima wangu umenifundisha usiku daima nimemweka Bwana mbele yangu kwa kuwa yuko kuumeni kwangu yuko kuumeni kwangu sitaondoshwa sitaondoshwa. 3. kwa kuwa moyo wangu unafurahi nao utukufu wangu unashangilia naam kwa kutumaini mwili wangu utakaa maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu. 4. Utanijulisha njia utanijulisha njia ya uzima mbele za uso wako zimo furaha tele na katika mkono wako wa kuu e mna mema mema ya milele mna mema ya milele.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa