Ingia / Jisajili

Tutengeneze Edeni Mpya

Mtunzi: F. E. Nyanza
> Tazama Nyimbo nyingine za F. E. Nyanza

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: David Niwagira

Umepakuliwa mara 62 | Umetazamwa mara 56

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

TUTENGENEZE EDENI MPYA (By F.Nyanza)

Dunia ilikuwa ni nzuri sana ilipotoka mikononi mwa Muumba, nchi ilikuwa yenye kijani kibichi, maua mazuri misitu, mimea ya kila aina na mito iliyo bubujika maji iliyo pamba dunia. Lakini kwa matokeo ya dhambi na kiburi cha mwanadamu, ameiharibu dunia na uzuri wake umetoweka.

Dunia imekuwa sikitiko

si mahali pazuri pa mimea,

mimea nayo mito ya asili

vingi vimetoweka

Dunia si rafiki tena kwa kizazi cha mwanadamu amejitengenezea kifo chake na kuiharibu hatima aliyo tengenezewa na Mungu.

Amekata miti,

kachoma misitu

kwa shughuli zake

za kila siku

ameyaharibu mazingira;

 

Iko wapi ile bustani ya Edeni ya kuvutia?

Iko wapi ile Dunia ambayo Mungu aliserma;

 

Tazama kila kitu ni chema (Ni chema) baada ya uumbaji wake.

Shime tuitengenezeni Edeni na kuurudisha uzuri wa dunia. Tuipande miti na kuvutia viumbe na tuwarithishe watoto urithi ulio mzuri. Pamoja tumpe Mungu utukufu na sifa kwa kazi yake.

 Basi na tusiiruhusu dunia iomboleze kutowajibika kwetu. Tutapata mvua, tukitunza mazingira tutayaepuka magonjwa na pia tutauepuka ukame na joto kali hakika vitatoweka duniani.

Tutengeneze Edeni mpya yawezekana kufanya hivyo,  jukumu langu mimi na wewe.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa