Maneno ya wimbo
Tuingie hekaluni.
Mwanzo
(Wakristu tuingie kwa furaha nyumba yake.) Tenor
(Nyumba yake tuingie tumtolee madhabihu.) sop&alto
Chorus
Tuingie hekaluni, tumwabudu mungu wetu, sala zetu na sadaka tumtolee atubariki.
1.Sote tuijongee nyumba yake mwenyezi, tukamwabudu mwamba wa wokovu wetu.
2.Hii ndiyo siku aliyoifanya bwana, tuifurahie na kuishangilia.
3.Makasisi tangazeni ukuu wake,
waamini shangilieni matendo ya bwana.
4.Ututakase ee baba tunakuja kwako,
sisi tu wakosefu twakuomba radhi.