Mtunzi: LUKRESIA MSELABUYE
> Mfahamu Zaidi LUKRESIA MSELABUYE
> Tazama Nyimbo nyingine za LUKRESIA MSELABUYE
Makundi Nyimbo: Tenzi za Kiswahili
Umepakiwa na: YOPASIA MSELABUYE
Umepakuliwa mara 1 | Umetazamwa mara 0
Download Nota Download MidiNIMEAMINI BY Lukresia Mselabuye
Verse 1.
Mungu ndiye muweza wa mambo yote eeeh
Nimechagua kuamini agabo lake kwangu
Japo kuwa napata vipingamizi
Nimechagua kusubiri ahadi zake kwangu
Wanayosema ni mengi kunirudisha nyuma
Lakini yote si kitu Nimesimama
Aliyotenda ni mengi Siwezi rudi nyuma
Siwezi kusimulia nikamaliza
Chorus!!
Soloist. Wote.
Kama Yesu ni mwanadamu. Sijui sijui sijui Ninasema
Ati Yesu mwana wa seremala. Sijui Sijui Sijui
Kama Yesu hakutoka kwa Mungu. Sijui sijui sijui Ninasema
Ati Yesu sio mwana wa Mungu. Sijui Sijui Sijui
Wote: Ninalijua moja nilikuwa kipofu sasa ninaona. ×2
Verse 2.
Ni Roho mtakatifu mwenye mapaji. iiiiiih
Nimechagua kutumaini nguvu zake kwangu
Ajuaye maana ya kila sauti
Nimechagua kuamini uwepo wake kwangu
Mwenye umungu mmoja na Mungu muumbaji
Mwenye ushirika kamili naye Yesu
Ninaamini ndani ya utatu mtakatifu
Ndipo napata uzima na nguvu tele
Chorus - Nalikuwa na dhambia nimesamehewa ×2
Verse 3
Eti kanisa usalipo sio la kweli iiiiih
Nimechagua kuamini kanisa moja tu
Kanisa katoriki na la mitume eeeeh
Msingi wake ndiye yesu mwokozi wetu
Alilojenga mwenyewe juu ya mwamba Petro
Nayo milango ya kuzimu haitashinda
Mashaka yao si kitu katika njia yangu
Nimeamini ninakiri Yesu ni Bwana
Chorus -Ninalijua moja nalifungwa na dhambi sasa nipo huru ×2
Verse 4
Eti maisha ulonayo hayakufai iiiih
Nimechagua kuamini ahadi zake kwangu
Ati ugonjwa ulonao hautapona aaah
Nimechagua kuamini mapenzi yake kwangu
Kuishi kwangu ni kristo na kufa ni faida
Najua kufanikiwa pia kudhiliwa
Nimefundishwa kushiba pia kuona njaa
Imani yangu kwake Yesu nimeiweka.
Chorus. . Ninalijua moja nalikuwa kiwete sasa natembea ×2
KIBWAGIZO.
Kwa maana jinsi hii
Mungu aliupenda ulimwengu wote
Kamtoa mwanae wa pekee
Ili kila amwaminiye asipotee
Bali awe na uzima wa milele
Ni upendo gani huu nimepewa
Yesu afe kwa ajili yangu mimi
Nimekombolewa kwa damu ya thamani
Yesu si mwanadamu
Hafananishwi na kitu
Kajivua utukufu
Afe kwa ajili yangu
Yesu kwangu ni Mungu
Mwana halisi wa Mungu
Sitaacha kulisifu
Jina lake lake takatifu Daima
Sifa apewe Bwana, sifa apewe Yesu Kristo
Sifa apewe Bwana Daima