Ingia / Jisajili

Najongea Na Zawadi

Mtunzi: B N Mogeni
> Mfahamu Zaidi B N Mogeni
> Tazama Nyimbo nyingine za B N Mogeni

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: Brian Mogeni

Umepakuliwa mara 1 | Umetazamwa mara 0

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

NAJONGEA NA ZAWADI

Najongea Bwana, na zawadi yangu nikukabidhi uipokee, unitakase na uovu wangu unibariki nipate zaidi. Nakuja na fedha, za mifuko na mazao ya shamba, pia naleta (nayo nafsi yangu (naomba) Bwana pokea x2)

Alto: Najongea na zawadi Bwana yangu mimi, nikukabidhi Bwana, uipokee. Unitakase Bwana na uovu, unibariki mimi, nipate zaidi Nakuja na fedha, za mifuko na mazao ya shamba, pia naleta (nayo nafsi yangu (naomba) Bwana pokea x2)

1.     Kama wawili walirudisha Bwana talanta zao, nami ninarudisha kusema asante Mungu.

2.     Kama ulivyoipokea, sadaka ya Ibrahimu, Abeli, Melkisedeki naomba Pokea yangu.

3.     Kama mmoja kati ya kumi, kaja kusema asante, na mimi nimerudi kusema asante Mungu.

4.     Vitu vyote ulivyonipa, Baba ninashukuru, tumaini langu kwako, leo hata milele.



Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa