Mtunzi: B N Mogeni
> Mfahamu Zaidi B N Mogeni
> Tazama Nyimbo nyingine za B N Mogeni
Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo
Umepakiwa na: Brian Mogeni
Umepakuliwa mara 1 | Umetazamwa mara 0
Download Nota Download Midi
NAJONGEA NA ZAWADI
Najongea Bwana, na zawadi yangu nikukabidhi uipokee, unitakase na uovu wangu unibariki nipate zaidi. Nakuja na fedha, za mifuko na mazao ya shamba, pia naleta (nayo nafsi yangu (naomba) Bwana pokea x2)
Alto: Najongea na zawadi Bwana yangu mimi, nikukabidhi Bwana, uipokee. Unitakase Bwana na uovu, unibariki mimi, nipate zaidi Nakuja na fedha, za mifuko na mazao ya shamba, pia naleta (nayo nafsi yangu (naomba) Bwana pokea x2)
1. Kama wawili walirudisha Bwana talanta zao, nami ninarudisha kusema asante Mungu.
2. Kama ulivyoipokea, sadaka ya Ibrahimu, Abeli, Melkisedeki naomba Pokea yangu.
3. Kama mmoja kati ya kumi, kaja kusema asante, na mimi nimerudi kusema asante Mungu.
4. Vitu vyote ulivyonipa, Baba ninashukuru, tumaini langu kwako, leo hata milele.