Ingia / Jisajili

Mwimbieni Bwana Zaburi

Mtunzi: Erick Mwaniki
> Tazama Nyimbo nyingine za Erick Mwaniki

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Shukrani

Umepakiwa na: Thomas George Mwakimata

Umepakuliwa mara 160 | Umetazamwa mara 519

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
MWIMBIENI BWANA ZABURI Mwimbieni Bwana zaburi watauwa wake Mwimbieni Bwana Na kufanya shukrani (kwa maana) Kwa kumbukumbu la utakatifu wake, nitamtukuza maana ameniinua, *2 Mwimbieni Bwana zaburi watauwa wake Mwimbieni Bwana Na kufanya shukrani 1. Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu (Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia (kulilia) Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya.) *2 2. Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu, kutoka kuzima, Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni. 3. Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha. Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. (Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele.)*2

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa