Maneno ya wimbo
                Mungu mpangaji
Eric Mwaniki FRANCIS, SJ
    1. Binadamu anapanga mambo mengi atakayofanya siku zijazo, 
       anawaza vyema na tena anatumia uzoefu alionao,
       atumaini, yote yatatimia 
       anaamini, yupo Mungu muweza
       
       Ni Mungu muumbaji wa mbingu na dunia aliyeweka vitu vyote pale vistahilivyo
       Mungu mpangaji wa mambo yaishiyo na mambo ya milele tumaini la mwanadamu
       
    2. Jumatatu hadi jumamosi anajishungulisha na utafutaji, 
       kisha siku ya saba anaamka na kuelekea madhabahuni,
       kumshukuru, yeye aliye juu, 
       na kumsifu, yeye Mungu muweza
       
    3. Anajishungulisha na familia yake kuwalea watoto wake
       wala hajishungulishi na mambo yanayoshinda ule uwezo wake 
       ye' anajua, Mungu ampigania 
       ye' ameweka, tumaini kwa Bwana
    4. Anajitenga na mabaya na dhambi kwani zina mkwaza Mungu wake,
       katika mambo mengi duniani anatamani moja tu litimie 
       anatamani, ampendeze Mungu 
       ili mwishoni, amlaki nyumbani
       
    5. Hata kwa magumu hafi moyo anamlilia Mungu mwenye uwezo,
       anajua kuwa hataaibika akimuita atamsikia
       atamjibu, kumfuta machozi
       nakumtia, nguvu na neema zake
            
                                    
                Nyimbo nyingine za mtunzi huyu