Ingia / Jisajili

Masikini Huyu Aliita Bwana Akasikia

Mtunzi: Joeli H.Kanyika
> Mfahamu Zaidi Joeli H.Kanyika

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Joeli Kanyika

Umepakuliwa mara 2 | Umetazamwa mara 0

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 30 Mwaka C

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio

Masikini huyu aliita Bwana akasikia×2

Mashairi

1. Nitamuhimidi Bwana kila wakati, sifa zake zi kinywani mwangu daima, katika Bwana nafsi yangu itajisifu, wanyenyekevu wasikie wakafurahi.

2. Uso wa Bwana ni Juu ya watenda mabaya, ili aliondoe kumbukumbu lao duniani, Walilia naye Bwana akasikia, akawaponya na tabu zao zote.

3. Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, na waliopondeka roho huwaokoa, Bwana huzikomboa nafsi za watumishi wake, wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa