Mtunzi: Eng.Richard Samson
> Mfahamu Zaidi Eng.Richard Samson
> Tazama Nyimbo nyingine za Eng.Richard Samson
Makundi Nyimbo: Kwaresma | Mafundisho / Tafakari | Zaburi
Umepakiwa na: Richard Samson
Umepakuliwa mara 1 | Umetazamwa mara 0
Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Dominika ya 3 Mwaka A
- Katikati Dominika ya 2 ya Kwaresma Mwaka C
Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Bwana ni nuru yangu na wokovu na wokovu wangu x2.
1. Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani?
Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?
2. Neno moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta,
Nikae nyumbani mwa Bwana, Siku zote za maisha yangu.
Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake.
3. Naamini ya kuwa nitauona wema wa Bwana, Katika nchi ya walio hai.
Umngoje Bwana, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje Bwana.