Ingia / Jisajili

Snob Mwinje

Mfahamu Snob Mwinje, mtunzi wa nyimbo za Kanisa Katoliki. Kutoka Jimbo la Dodoma Parokia ya Manda

Maelezo zaidi

Idadi ya nyimbo SMN: 34 > Zitazame

Jimbo analofanya utume: Dodoma

Parokia anayofanya utume: Manda

Namba ya simu: Halotel:0629254075 tiGo:0679254075

Soma Historia na maelezo yake hapa

Wasiliana na mtunzi kwa email:


Historia / Maelezo

Mimi ni mtoto wa kwanza kwa Baba Damian Mwinje na Mama Veronica Fundi. Familia yetu ina jumla ya watoto sita, wanaume 3 na wanawake 3, lakini pia Baba ana mtoto mmoja wa kike, na Mama naye pia ana mtoto mmoja wa kike hivyo jumla tuko nane. Mimi ni mkazi wa Dodoma na kabila langu ni Mgogo, watani zangu wakubwa ni Wasukuma. Nilihitimu shule ya msingi mwaka 2008 katika shule ya msingi ya kijijini kwetu Chifutuka, na shule ya upili yaani 'secondary School' nikahitimu mwaka 2012 katika shule ya kata ya Chifutuka iitwayo Magaga Sec. School. Hivyo elimu yangu ni kidato cha nne. Nilijifunza muziki kwa Katekista Wilbert Lugobi mwaka 2017 nikaanza kusovu nyimbo na kufundisha Kwaya mbalibali ikiwemo kwaya ya nyumbani ya Mwenye heri Sr. Irene Stefano ya Kigango Cha Mt. Mathayo Chifutuka. Mnamo mwaka 2022 - 2023 nilienda Chuo Cha CTC Makalala nikajifunza zaidi Muziki Mtakatifu kwa Level I - IV na mwalimu Fr. George Paul Kulwa Sayi wa SDB aliyekuwa Mkurugenzi wa Chuo hicho kwa miaka hiyo. Kwa kifupi hiyo ndo safari yangu ya muziki mpaka kufikia hivi leo. Asanteni nyote.