Ingia / Jisajili

Tuwe Naye Milele

Mtunzi: Ronaldo Nakaka
> Mfahamu Zaidi Ronaldo Nakaka
> Tazama Nyimbo nyingine za Ronaldo Nakaka

Makundi Nyimbo: Tenzi za Kiswahili

Umepakiwa na: Vusile Silonda

Umepakuliwa mara 680 | Umetazamwa mara 2,488

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
1.E nyi wa Mungu wana wa pendwa
E nyi kwa Jina la ke , walindwa
E nyi wa Kri sto m na o mwa mi ni
Mungu Mwana kumtumaini
Gharama yenu sana adhimu
Ndi yo ya mwa na ko ndoo da mu
A liye wa a ndi ke ni hu ru
Toka giza kwenda  kwenye nuru
 
Kiitikio
A me tu i ta
A me tu ta ka sa
A ta tu chu ku a
Tu we na ye mi le le
 
2. Si kwa nguvu za wetu mwili
Si ujuzi wa zetu akili
Bali ni kwa nyingi rehema
Ni kwa Roho wa neema
Yeye mwenyewe katupa haki
Japo Mjaribu atushitaki
Hakimu ndiye Baba yetu
Katuhesabu watakatifu
 
3. Sio kama kuf'ata sharia
Ni nyepesi yake nira
Roho wake daima dira
Moyoni kweli hushuhudia
Kwani jibebesha zigo zito?
Matendo mwili changamoto
Wakati Rabi ataka utua
Pekeyo tashindwa taungua
 
 
 
4. Sheria yake kuu ni Upendo
Imani na uchaji mwenendo
Kwa Muumba na kwake jirani
Huruma, wema na hisani
Kama Baba anavyorehemu
Na kama anavyotukirimu
Nasi tukasamehe watesi
Nakutoa kwa moyo mwepesi

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa