Ingia / Jisajili

Noeli Ya Kwanza (Malaika Kaleta)

Mtunzi: Traditional
> Tazama Nyimbo nyingine za Traditional

Makundi Nyimbo: Noeli

Umepakiwa na: Thomas George Mwakimata

Umepakuliwa mara 8,228 | Umetazamwa mara 13,270

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

1. Malaika kaleta noeli ya kwanza kwa wachunga kondoo katika makonde, Betlehemu wakawa walinzi wazamu wakaona usiku maajabu ya nuru, (Noeli, Noeli, Noeli Yesu yu Mungu na binadamu) x 2.

2. Wakaona Mbinguni mwangaza wa nyota, Ing'aayo kwa mbali na masharikini, wakaenda upesi walivyoambiwa, Betlehemu wamwone mwokozi horini, Noeli, noeli..........................................

3. Mashariki watoka Wafalme watatu, Mamajusi waliotafuta Mfalme, Wafuata hii nyota walioiona, wasipate kumkosa wanayemtafuta. Noeli, Noeli.......................

4. Kiongozi ni nyota iliyowaleta hata mji wa Daudi alimozaliwa, Ikakaa mara moja isiendelee, palepale nyumbani alimo mwokozi, Noeli, Noeli................................

5. Basi sisi Wakristu na tumsujudie, tumhimidi Mwokozi aliyeviumba vitu vyote Mbinguni duniani, na sisi ametufia na kutukomboa, Noeli, Noeli...................................................


Maoni - Toa Maoni

PROSPER YALUTINDI Dec 04, 2017
safi saaana...wimbo umetumwa kama ulivyo

Toa Maoni yako hapa