Ingia / Jisajili

Nitamwimbia Bwana

Mtunzi: Joseph Rimisho
> Mfahamu Zaidi Joseph Rimisho
> Tazama Nyimbo nyingine za Joseph Rimisho

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Shukrani

Umepakiwa na: JOSEPH RIMISHO

Umepakuliwa mara 1,319 | Umetazamwa mara 4,274

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Kiitikio

Nitamuimbia Bwana Mungu wangu ningali hai,

Nitautangaza utukufu wake kwa mataifa

(NItavipiga vinanda, nitazicheza na ngoma, nitavicheza vinubi, nitalicheza na zeze (nami)

Nitasimulia maajabu ya Mungu kwa viumbe vyote) x2

Mashairi

1.(a). Katika kundi kubwa nitatangaza sifa zake,

    (b). Nitamsifu kwa matari na kwa filimbi tamu, nitawaongoza watu wamtukuze Bwana Mungu wetu.

2. (a). Enyi jamaa za dunia msifuni kwa shangwe,

    (b). Muimbieni Mungu wetu aliye juu mbinguni, mtukuzeni katika utakatifu na ukuu wake.

3. (a). Moyo wangu ni chombo kilichojaa sifa yake,

    (b). Ulimi wangu utakiri matendo yake Mungu, na nafsi yangu itayasifia matendo yake Mungu wetu.


Maoni - Toa Maoni

Elias Boniface Mar 02, 2019
Hongera sana kwa wimbo mzuri ....mashairi yananijenga sana kiroho na kimwili

Toa Maoni yako hapa