Ingia / Jisajili

Nimekukimbilia Wewe Bwana

Mtunzi: Alfred Ogombo
> Mfahamu Zaidi Alfred Ogombo
> Tazama Nyimbo nyingine za Alfred Ogombo

Makundi Nyimbo: Kwaresma

Umepakiwa na: Alfred Ogombo

Umepakuliwa mara 656 | Umetazamwa mara 2,671

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Nimekukimbilia Wewe Bwana, nisiaibike milele kwa haki yako 'niponye,

Mikononi mwako Bwana naiweka roho yangu

1.Kwasababu ya watesi wangu nimekuwa laumu

   Naam hasa naam hasa kwa jirani zangu

   Nimekuwa kitu cha kutisha kwa rafiki zangu,

   Walioniona njiani walinikimbia

2.Nimesahauliwa kama mfu asiyekumbukwa,

   Nimekuwa kama chombo kilichovunjika

   Maana nimesikia masingizio ya wengi,

   Hofu ziko hofu ziko hofu zi’ pande zote

3.Lakini mimi ninakutumaini Wewe Bwana

   Nimesema Wewe ndiwe ndiwe Mungu wangu

   Nyakati zangu ee Bwana zimo mikononi mwako

   ’niponye na’dui zangu nao wan’onifuatia

4.Umwangaze mtumishi wako kwa nuru ya uso wako

   Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako

   Iweni hodari hodari mpige moyo konde,

   Ninyi nyote ninyi nyote mnaomngoja Bwana


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa