Ingia / Jisajili

Ndama Wa Nono

Mtunzi: Faustine J. Mtegeta
> Tazama Nyimbo nyingine za Faustine J. Mtegeta

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: Yudathadei Chitopela

Umepakuliwa mara 19,345 | Umetazamwa mara 27,406

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Leteni ndama walionona madhabahuni kwa Bwana tena toeni bila kinyongo moyoni ndipo mtabarikiwa naye x 2

1.      Leteni ndama aliyeshiba majani ya kondeni, mkamtolee Mungu Baba yenu kwa shukrani.

2.      Peleka sadaka yako iliyo safi na ya kupendeza, ndipo utakapokitikisa kiti cha mwenyezi.

3.      Kumbuka yule mjane aliyetoa senti moja, alibarikiwa na kuongezewa na mwenyezi.

4.      Sadaka iliyo safi ni ile inayokugusa wewe, hiyo ndiyo sadaka iliyo safi sana.

5.      Isaka alitolewa na baba yake kama sadaka, hivyo Abrahamu alizidishiwa uzao wake.


Maoni - Toa Maoni

Rose beda joseph Jan 06, 2024
Nyimbo ni nzuri sana

Br. Stan Mkombo Jul 20, 2017
Ndugu Mtegeta, kwanza hongera kwa mchango wako mkubwa na wa siku nying kwa tasnia ya muziki wa liturjia hapa Tanzania. Pia kwa wimbo huu Ndama Wanono, au Ndama Walionona. Lbada pendekezo tu fupi kuhusu Shairi la Pili la Wimbo huu: Unaonaje kama lingeishia "Ndipo utakapokifikia kiti cha Mwenyezi" badala ya "Ndipo utakapo 'kitikisa' ...", kwa kuwa kidogo kukitikisa kiti cha Mwenyezi kiteolojia haiendi vizuri sana kwa kuwa kiti cha Mungu hakiwezi kutikisika. Maana "Amejivika na Kujikaza Nguvu".

Glory Jul 18, 2017
Wimbo ni mzur sana, nilikuwa naomba audio na video pia muweke

Toa Maoni yako hapa