Ingia / Jisajili

Na Ahimidiwe Bwana

Mtunzi: Paschal Florian Mwarabu
> Tazama Nyimbo nyingine za Paschal Florian Mwarabu

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Martin Munywoki

Umepakuliwa mara 2,784 | Umetazamwa mara 6,989

Download Nota
Maneno ya wimbo

Enyi Watumishi wa Bwana

Enyi watumishi wa Bwana sifuni

Lisifuni lisifuni Jina la Bwana

Na ahimidiwe Bwana Mungu

Bwana Mungu kutoka Sayuni

Akaaye Yerusalemu aleluya

1.     Ninyi msimamao nyumbani mwa Bwana

  Nyuani mwa nyumba ya Mungu wenu

  Msifuni Bwana kwa kuwa yu mwema

  Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza

2.  Kwa sababu Bwana amejichagulia Yakobo

  Na Israeli wawe watu wake hasa

  Maana najua mimi ya kuwa Bwana ni mkuu

  Na Mungu wetu yu juu ya miungu yote

3.  Enyi mlango wa Israeli mhimidini

  Enyi mlango wa Haruni mhimidini

  Enyi mlango wa Lawi mhimidini Bwana

  Enyi mnaomcha Bwana mhimidini Bwana


Maoni - Toa Maoni

Anselm Namala Sep 19, 2019
Hongereni sana..hii ndo sehemu pekee mimi huja na kupata faraja kwa nyimbo na mafundisho..Mungu awabariki sana

pius phinias Dec 14, 2016
Mungu azidi kukubariki Tunu ya Kanisa Mzee P.F. Mwarabu. Tungo zako zinanibariki sana.

Toa Maoni yako hapa