Ingia / Jisajili

Mungu Mmoja Wa Kweli

Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Vusile Silonda

Umepakuliwa mara 562 | Umetazamwa mara 2,530

Download Nota
Maneno ya wimbo

Siyo sisi Ee Mungu, siyo sisi bali wewe peke yako utukuzwe. Kwa nini mataifa wanatuuliza Mungu wenu yuko wapi? Mungu wenu yuko wapi? Mungu wetu yuko mbinguni Aleluya! Yeye hufanya atakalo Aleluya!

  1. Sanamu zao zimejengwa kwa fedha na dhahabu, zimetengenezwa kwa mikono, mikono yao wanadamu, zina vinywa haziwezi kusema, zina macho haziwezi kuona, zina masikio haziwezi kusikia, zina pua haziwezi kunusa zina mikono haziwezi kupapasa, zina miguu haziwezi kutembea, wala koo zao haziwezi, haziwezi kutoa sauti, wale wanaozitengeneza watafanana zao vivyo hivyo na wale wote watakaozitumainia.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa