Ingia / Jisajili

Mbarikiwa Yosefu Allamano Utuombee

Mtunzi: Chris Oyier
> Mfahamu Zaidi Chris Oyier
> Tazama Nyimbo nyingine za Chris Oyier

Makundi Nyimbo: Watakatifu

Umepakiwa na: CHRIS OYIER

Umepakuliwa mara 311 | Umetazamwa mara 1,755

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

MBARIKIWA YOSEFU ALLAMANO UTUOMBEE

1.

Mbarikiwa Yosefu Allamano, uliye somo wetu, tunakusihi, utuombee kwa Mungu Baba.

Katika safari yetu ya utakatifu, utuombee sisi, tuweze kufuata njia kutufikisha kwa Mungu.

Tuwe Watakatifu kabla kuwa Wamishonari, tuwe Watakatifu kabla kuwa wanakwaya, tuwe Watakatifu kabla kuwa viongozi wa kanisa, ulitufunza, kuwa utakatifu huja, kabla kuwasaidia wengine kuwa watakatifu. Huwezi kupeana kile ambacho huna.

2.

Mbarikiwa Yosefu Allamano, uliye somo wetu, tunakusihi, utuombee kwa Mungu Baba.

Katika safari yetu ya utakatifu, utuombee sisi, tuweze kufuata njia kutufikisha kwa Mungu.

Nyoyo zetu zitaokolewa kwa utakatifu, sote tuokolewe mwisho tumuone Mungu, maishani tufanye kila kitu vyema pia iwe siri, ulitufunza, tumuige Mungu kwa yote, tutakuwa tumeishi maisha ya utakatifu, maisha yetu yawe funzo, utakatifu.

3.

Mbarikiwa Yosefu Allamano, uliye somo wetu, tunakusihi, utuombee kwa Mungu Baba.

Katika safari yetu ya utakatifu, utuombee sisi, tuweze kufuata njia kutufikisha kwa Mungu.

Ulivyomsikiza Mama wa Consolata mkaanzisha, shirika la kimishonari la Consolata, tufanye kazi pamoja kueneza injili yake Mungu, ulitufunza, hekima huja kwa shauri, ushauri ni umoja kufanya kazi yake Mungu. Tushirikiane katika kazi ya Mungu.

Nyimbo nyingine za mtunzi huyu

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa