Ingia / Jisajili

Kioo Ni Yesu

Mtunzi: Chris Oyier
> Mfahamu Zaidi Chris Oyier
> Tazama Nyimbo nyingine za Chris Oyier

Makundi Nyimbo: Tenzi za Kiswahili

Umepakiwa na: CHRIS OYIER

Umepakuliwa mara 696 | Umetazamwa mara 2,490

Download Nota
Maneno ya wimbo

KIOO NI YESU - Na Chris Oyier

 

Nimefunuliwa jambo moja, jambo hilo waziwazi.

Lipi,  kipi, wapi, jambo hilo, jambo hilo ni kioo.

(Kioo,  kioo,  kioo,  kioo,  kioo) Kioo huyu ni Yesu. (Je wajua Yesu ni kioo) tega sikio ujue.  >>>>

 

1. Yesu kazaliwa Bethlehemu horini mwa ng'ombe, kawacha ufalme wake, kaunganika na udhaifu , wa mwanadamu, mateso hapa duniani.

(Kwa hivyo), kioo ni kuunganika na wale wasojiweza, wape matumaini, na kuwasaidia.

2. Mfalme Herode kwa hofu alipanga kumuua Yesu, Malaika akatumwa,  kamwambia Yosefu torosha,  Maria na Yesu, wasidhurike na Herode.

(Kwa hivyo) kioo ni kuisikia sauti ya Mungu wetu,  kumuamini yeye,  kuwa atulinda vyema.

3. Yesu kafunga jangwani shetani kamjaribu, akamshinda shetani, kwa nguvu za Mungu Baba yake, akapata roho, kufa kwa dhambi zetu.

(Kwa hivyo) kioo ni kumtumaini Mungu atupe nguvu, kushinda majaribu,  na maovu ya dunia.

4. Yesu kafanya miujiza kahubiria watu, kaonesha mfano bora, kwake kusali kila wakati,  kuwa mtumishi,  kukomboa wanadamu.

(Kwa hivyo) kioo ni kusali kila wakati bila kukoma, sote kujitolea, kufanya kazi ya Mungu.

5. Yesu alikataliwa na akasulibiwa,  kwa makosa yetu sisi, akafa na pia kafufuka, kashinda mauti,  katukomboa dhambini.

(Kwa hivyo ) kioo ni kuvumilia mateso na kusimangwa, mwisho tavikwa taji, ya uzima wa milele.

 

 

Nyimbo nyingine za mtunzi huyu

Maoni - Toa Maoni

Gilbert Mar 25, 2017
214

Toa Maoni yako hapa