Ingia / Jisajili

Kimya Namngoja Mungu

Mtunzi: Br. Emmanuel Mwita, Ofmcap.
> Mfahamu Zaidi Br. Emmanuel Mwita, Ofmcap.
> Tazama Nyimbo nyingine za Br. Emmanuel Mwita, Ofmcap.

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Emmanuel Mwita

Umepakuliwa mara 372 | Umetazamwa mara 1,451

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

                                            KIMYA NAMNGOJA MUNGU

1.      Nafsi yangu yamngoja, Mungu peke yake kwa kimya, wokovu wokovu wangu, hutoka kwake;

         Yeye tu ndiye mwamba, mwamba wangu na wokovu wangu, ngome yangu ngome yangu, sitatikisika sana.

                    Kimya kimya nafsi yangu, yamngoja Mungu, kimya kimya yamngoja, Mungu peke yake x2

2.      Nafsi yangu umngoje Mungu, Mungu peke yake kwa kimya, tumaini tumaini langu, hutoka kwake;

         Yeye tu ndiye mwamba wangu, na wokovu wangu, ngome yangu ngome yangu, sitatikisika sana.

3.      Kwa Mungu wokovu wangu, na utukufu wangu, mwamba wa nguvu zangu, na kimbilio langu ni kwa Mungu;

         Enyi watu mtumaini, mtumaini siku zote, ifunueni mioyo yenu, Mungu ndiye kimbilio letu.

Nyimbo nyingine za mtunzi huyu

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa