Ingia / Jisajili

Kilio Changu

Mtunzi: Felician Albert Nyundo
> Tazama Nyimbo nyingine za Felician Albert Nyundo

Makundi Nyimbo: Tenzi za Kiswahili

Umepakiwa na: Yudathadei Chitopela

Umepakuliwa mara 2,075 | Umetazamwa mara 6,345

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

1.      Kilio changu ukikisikia, ufanye haraka kunisaidia,

Na pindi shida zinaponijia, ufanye haraka kunisaidia.

2.      Ee Mungu wangu, ndiwe kimbilio, Ewe Bwana wangu, ndiwe tegemeo.
Nikitaabika uje kwangu mbio, Ewe ngome yangu, njoo kwangu, njoo.

3.      Usinitupe wewe ndiwe kinga, Mimi ni kondoo, wewe wanichunga.
Adui zangu zidi kuwapinga, Na giza likija, nipatie mwanga.

4.      Daima wewe ni wangu msaada, Bwana, usichoke zidi kunilinda.
Ukiwa nami sitapata shida, Kwa uwezo wako, mimi nitashinda,

5.      Uniepushe na mwovu shetani, Ili asinitie majaribuni.
Mimi mnyonge nakutumaini, Wewe uwe nami, nifike mbinguni.


Maoni - Toa Maoni

EMMANUELY TENSON KASANGA Sep 11, 2016
Hongera sana mtunzi kwa ujumbe wako mzuri bwana akubariki sana

Toa Maoni yako hapa