Ingia / Jisajili

Karibu Mwokozi

Mtunzi: N. E. Kisima
> Tazama Nyimbo nyingine za N. E. Kisima

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio | Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Yudathadei Chitopela

Umepakuliwa mara 13,838 | Umetazamwa mara 23,681

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

1.       a) Ee Mwokozi ninakukaribisha uje kwangu uwe nami daima ni wewe uliye utimilifu wewe ndiwe Kristo Mwana wa Mungu

b) Ndiwe njia ukweli na uzima nuru halisi ishindayo giza, ukanipe uzima wa milele ndio kuwa na wewe maishani

       CHORUS

                Karibu kwangu (mwokozi) Ee Mwokozi uje kwangu (uje mwokozi)

                Karibu kwangu (mwokozi) Ee Mwokozi uwe nami

2.       a) Unijaze hekima ile kuu uliyokuwa nayo Ee Mwokozi nikaishi upendo na utii na unyenyekevu maishani

b) Ukanipe akili ile kuu nikaseme karika mambo yote Baba mapenzi yako yatimizwe siku zote maishani mwangu

3.       a)Maumbo ya mkate na divai fumbo kuu hilo la Ekaristi ndimo ulimoacha ukumbusho wa kujitoa kwako tuokoke

b) Sema neno tu nasi tutapona kwani wewe u neno wake Baba kwa neno lake Baba tutaishi na wewe u neno wake Baba

4.       a)Ukanipe na usafi wa moyo nikamwone Mungu Baba milele ndiyo  hamu niliyo nayo mimi kuonana nae uso kwa uso

b) Utukuzwe Mungu Baba muumba nawe mwana mwokozi wa dunia nawe roho mtakatifu milele hata milele. Amina


Maoni - Toa Maoni

Upendo Jul 04, 2022
Mungu awabariki uinjilishaji mzuri sana huu, ila tunaomba tupate audio

SUNDAY BEEBWA Sep 16, 2020
Tunabarikiwa sana na Tovuti hii

stamphord kinyamaishwa Jul 06, 2018
Nafurahi sana naposikiliza nyimbo zako mungu akubariki

Amos edward Jul 12, 2016
PongezI; wimbo wako nimeupenda sana tena munu yaan unanipa hamasa kubwa moyoni mwangu. mungu akubaliki sana kama unazonymbo zngne nitumie kwenye hyo email ambazo znatafakari nzito.

Toa Maoni yako hapa