Ingia / Jisajili

Ee Mungu Mkuu - Bwana Asifiwe Na Viumbe

Mtunzi: Fr. Gregory F. Kayeta
> Tazama Nyimbo nyingine za Fr. Gregory F. Kayeta

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari | Watakatifu | Shukrani

Umepakiwa na: Stanslaus Mkombo

Umepakuliwa mara 5,060 | Umetazamwa mara 12,490

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

EE MUNGU MKUU                                        [Fr. G.  F. Kayetta]

//Ee Mungu Mkuu, mwema na Mwenyezi, sifa ni zako, utukufu na heshima; ewe Bwana usifiwe siku zote na viumbe vyako vyote.//

1.         Usifiwe, ee Bwana, na Ndugu Jua, ang’ara kwa fahari kutuangaza, na siku zote     akutangaza      wewe Mkuu.

2.         Usifiwe ee Bwana, na Dada Mwezi, na Nyota za angani ulizoweka, Angavu nazo nzuri     mno zakusifu wewe.

3.         Usifiwe ee Bwana na Ndugu Upepo, na hewa, na mawingu, majira yote. Hivyo wawapa   chakula viumbe wako wote

4.         Usifiwe Ee Bwana na Dada majii, Usifiwe ee Bwana na Ndugu Moto; Vyote vyatufaa     sana, vya thamani kubwa.

5.         Usifiwe ee Bwana, na Mama Ardhi, atupaye riziki, na kutulisha, kwa matunda na maua     na        majani yote.

6.         Usifiwe Ee Bwana na wale wote, Ambao husamehe wenzao wote, Na kuvumilia   magonjwa        na masumbuko.

7.         Usifiwe ee Bwana na Dada Mauti, ambaye mwanadamu awaye yote, hawezi kamwe         kumuepa Dada huyo.

8.         Enyi viumbe vyote mtukuzeni Bwana, Msifuni Bwana wangu, mshukuruni wote,   Mtumikieni kwa unyenyekevu mkubwa.


Maoni - Toa Maoni

Gaudensia Emanuel Nov 04, 2020
Wimbo mzuri sana. Nimeomba audio yake tafadhali ??

Andrea Samsoni Chacha Sep 04, 2016
Ni Nazi nzuri sana mnayofanya

Toa Maoni yako hapa