Ingia / Jisajili

Chakula Kitokacho Mbinguni

Mtunzi: J. Mgango

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio

Umepakiwa na: Joseph Isaya Mwakapila

Umepakuliwa mara 1,754 | Umetazamwa mara 4,101

Download Nota
Maneno ya wimbo

Ninapo kula mwili wako Ee Bwana moyoni (Bwana) mwangu hujaa furaha

Ninapokunywa damu yako Ee Bwana moyoni (Bwana) mwangu hujaa furaha

Chakula hiki Bwana kitokacho mbinguni Kinywaji hiki Bwana kitokacho mbinguni kweli ni uzima Bwana nipe siku zote ukae ndani yangu Bwana nami ndani mwako milele na milele x2

1.       Nilishe Bwana ninakuomba, Ninyweshe Bwana ninakuomba, Chakula hiki Bwana chenye uzima (uzima) wa milele

2.        Bahati gani nimeipata, Kufika hapa altareni, nile Chakula (Bwana) chenye uzima wa milele.

3.        Ninatamani niwe na wewe, Nimejongea kwenye karamu, nile Chakula (Bwana) chenye uzima wa milele.

4.       Huruma Bwana msaada wako, Ninakuomba kwa moyo wote, nile Chakula (Bwana) chenye uzima wa milele.

5.       Ingia Bwana ndani mwangu, Niwe wako siku zote, nipe Chakula (Bwana) chenye uzima wa milele


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa