Ingia / Jisajili

Aleluya Mt Mikaeli

Mtunzi: Michael Matai
> Mfahamu Zaidi Michael Matai
> Tazama Nyimbo nyingine za Michael Matai

Makundi Nyimbo: Pasaka

Umepakiwa na: Michael Matai

Umepakuliwa mara 1,209 | Umetazamwa mara 3,801

Download Nota
Maneno ya wimbo

Aleluya, Aleluya!

Vijilia ya Pasaka.

1. Mshukuruni Bwana kwakuwa ni mwema, Kwamaana fadhili zake ni za milele/ Israeli na aseme sasa, ya kwamba fadhili zake ni za milele.

2. Mkono wa kuume wa Bwana umetukuka, mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu/ Sitakufa bali nitaishi, nami nitayasimulia matendo ya Bwana.

3. Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni/ Neno hili limetoka kwa Bwana, nalo ni ajabu machoni petu!

Dominika ya Pasaka.

Kristu pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka/ Basi na tuifanye karamu katika Bwana.

Dominika za kawaida.

1. Nena Bwana, kwakuwa mtumishi wako anasikia/ Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.

2. Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ayatie nuru macho ya mioyo yetu/ ili tujue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa